• Welcome

  • TANROADS YATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI MKUU

    TANROADS YATEKELEZA AGIZO LA WAZIRI MKUU

  • MABORESHO YALIYOFANYWA NA TANROADS KWENYE MIZANI YADHIBITI MIANYA YA RUSHWA -  MHANDISI KYAMBA

    MABORESHO YALIYOFANYWA NA TANROADS KWENYE MIZANI YADHIBITI MIANYA YA RUSHWA -  MHANDISI KYAMBA

  • TANROADS YAAGIZWA KUWEKA MAGETI MAENEO INAPOKUTANA RELI NA BARABARA

    TANROADS YAAGIZWA KUWEKA MAGETI MAENEO INAPOKUTANA RELI NA BARABARA

  • KASEKENYA AELEKEZA TANROADS KUHAKIKISHA MAWASILIANO YANAREJEA MALINYI

    KASEKENYA AELEKEZA TANROADS KUHAKIKISHA MAWASILIANO YANAREJEA MALINYI

  • WANANCHI WAIPONGEZA TANROADS-MOROGORO KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA WILAYANI MALINYI

    WANANCHI WAIPONGEZA TANROADS-MOROGORO KWA KUREJESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA WILAYANI MALINYI

  • BIL 97.178 KUTUMIKA UJENZI BARABARA YA IFAKARA-MBINGU

    BIL 97.178 KUTUMIKA UJENZI BARABARA YA IFAKARA-MBINGU

  • TANROADS YAWEKA KAMBI BARABARA YA MOROGORO- IRINGA KUZIBA MASHIMO MAENEO YALIYOHARIBIWA NA MVUA

    TANROADS YAWEKA KAMBI BARABARA YA MOROGORO- IRINGA KUZIBA MASHIMO MAENEO YALIYOHARIBIWA NA MVUA

  • TANROADS YAENDELEA NA KAZI YA KUZIBA MASHIMO YALIYOTOKEZA KATIKA BARABARA YA MOROGORO- IRINGA KUTOKANA NA MVUA KUBWA ZINAZOENDELEA KUNYESHA

    TANROADS YAENDELEA NA KAZI YA KUZIBA MASHIMO YALIYOTOKEZA KATIKA BARABARA YA MOROGORO- IRINGA KUTOKANA NA MVUA KUBWA ZINAZOENDELEA KUNYESHA

  • KATIBU MKUU UJENZI AZITAKA TAASISI ZOTE ZIANZE KUTUMIA MFUMO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI

    KATIBU MKUU UJENZI AZITAKA TAASISI ZOTE ZIANZE KUTUMIA MFUMO WA UFUATILIAJI NA TATHMINI

  • Serikali yaendelea kutekeleza miradi ya Kitaifa mkoani Morogoro

    Serikali yaendelea kutekeleza miradi ya Kitaifa mkoani Morogoro

  • TANROADS MBIONI KUKAMILISHA MIRADI WA MIZANI YA KISASA MIKUMI MKOANI MOROGORO

    Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia TANROADS ipo mbioni kukamilisha ujenzi wa Mizani mipya wa kisasa wa Mikumi uliopo barabara kuu ya Morogoro - Iringa, pamoja na maboresho katika mizani ya mikese uelekeo wa barabara ya Dar-es Salaam - Morogoro kwa gharama ya shilingi bilioni 1.9, hatua ambayo itakayosaidia kumaliza msongamano wa magari katika barabara hizo.
    Mwakilishi wa Meneja wa TANROADS mkoa wa Morogoro Mhandisi Mussa Kaswahili amesema hayo tarehe 18 Julai 2023, alipozungumza na vyombo vya habari kwa niaba ya Meneja wa TANROADS wa mkoa huo Mhandisi Alinanuswe L. Kyamba mara baada kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Mizani hiyo ambao kwa sasa umefikia asilimia 80.
    Amesema baada ya kuongezeka kwa shughuli za uzalishaji na Usafirishaji katika barabara ya TANZAM Highway, Serikali iliona Mzani uliopo kwa sasa hautoshelezi mahitaji ya kupima magari kwa wingi, hivyo imeamua kufanya maboresho ya mzani uliopo pamoja na kujenga Mzani mwingine mpya na wa kisasa ili kuendana na mahitaji ya sasa.
    Amesema maboresho yanayofanyika katika mizani hizo mbili ni pamoja na kuweka vifaa maalum [Sensor] ambavyo vitafanya kazi ya kuchuja na kutoa taarifa ya uzito wa gari husika, kama limezidisha mzigo ama la na kama halikuzidisha basi linaendelea na safari moja kwa moja bila kupita katika Mzani na lile lililozidisha mzigo litalazimika kupita kwenye mzani.
    Mhandisi Kaswahili amemtaja Mkandarasi wa mradi huo ni Kampuni ya kizalendo CGI Construction Company Limited ya mjini Morogoro ambayo imepewa kazi hiyo mwezi Februari mwaka huu na inatarajiwa kukamilisha mradi tarehe 30 Septemba 2023.
    "TANROADS inapenda kuishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hasaan kwa kuendelea kuwa karibu na Wananchi kwa kutenga fedha na kuzileta kwa ajili ya matengenezo kwenye maeneo yenye changamoto, lengo la upimaji wa magari ni kudhibiti uzito ili barabara zetu ziweze kudumu, natoa wito kwa Wananchi hasa wasafirishaji kutoa ushirikiano katika kutunza na kulinda barabara zetu" Amesisitiza Mhandisi Kaswahili.
    Ameongeza kuwa TANROADS na Serikali haijivunii kuwa na tozo nyingi katika mizani "tunavyotoza kwa wanaozidisha mzigo tunataka kuondosha magari yenye uzito mkubwa ili kulinda barabara zetu ambazo tumejenga kwa gharama kubwa kwa fedha zetu wenyewe, tunataka watu watii na kufuata sheria".
    Nao baadhi ya Madereva wanaotumia barabara hiyo Ismail Madunda na Vincent Mkimbila wamesema kukamilika kwa maboresho na ujenzi wa mizani mpya Mikumi kutasaidia kumaliza msongamano katika maeneo hayo na hivyo kuwafanya wasafiri na wasafirishaji kufika kwenye safari zao kwa wakati.
    Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa eneo hilo Bwana Antony Michael amesema "Tunaushukuru uongozi wa Rais Samia kwa kutujengea mizani mpya na maboresho yanayofanyika hapa, mradi huu ukikamilika foleni hapa itakuwa byee byee na watu watafika kwenye shughuli zao mapema kabisa".

  • Mafunzo maalum yaliyolenga Uzingatiaji Sheria, Kanuni, Taratibu katika Utendaji wao wa kazi hususan katika Masuala ya Nidhamu

    Wafanyakazi wa Wakala ya Barabara Tanzania wameshiriki Mafunzo  maalum yaliyolenga Uzingatiaji Sheria, Kanuni, Taratibu katika Utendaji wao wa kazi hususan katika Masuala ya Nidhamu na kufanyika katika Ukumbi wa TAFORI, Mkoani Morogoro.
    Mafunzo hayo ya siku mbili kuanzia Januari 28 hadi 29 yaliandaliwa na Tume ya Utumishi wa Umma.
    Miongoni mwa Washiriki wa Mafunzo hayo ni Mameneja wa Mikoa, Baadhi ya Wakuu wa Vitengo vya Uhasibu na Utawala pamoja  na Wawakilishi wa Chama cha Wafanyakazi (TAMICO) wa Makao Makuu na Mikoa.

    Mafunzo hayo yalifunguliwa na Mkurugenzi wa Huduma za Uendeshaji Bwana Hija Ally Malamla.

  • WANAWAKE WAASWA KUCHANGAMKIA KAZI ZA BARABARA

    Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano imesema itahakikisha wanawake walio katika Sekta ya Uhandisi na Ukandarasi wanapata fursa za kusimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya ujenzi na matengenezo ya barabara.

  • WANAWAKE KUPEWA KIPAUMBELE MIRADI YA UJENZI

    WANAWAKE  KUPEWA KIPAUMBELE  MIRADI  YA UJENZI

  • UJENZI WA BARABARA YA KIDATU-IFAKARA KUKUZA UCHUMI WA MOROGORO

    Serikali imesema imeanza ujenzi wa barabara ya Kidatu-Ifakara yenye urefu wa KM 66.9 kwa kiwango cha lami ambapo kukamilika kwake kutachochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika wilaya za mkoa wa Morogoro.