• Welcome

  • BARABARA ZA LAMI KIGOMA KUONGEZEKA

     

  • KIWANJA CHA NDEGE KIGOMA KULETA FURSA ZA UWEKEZAJI

    Baada ya kukamilika kwa zoezi la Utiaji Saini Mkataba wa Ujenzi wa Jengo la Abiria na Mnara wa Kuongozea Ndege katika Kiwanja cha Ndege cha Kigoma, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa alipata nafasi ya kuzungumzia uboreshaji wa kiwanja cha ndege cha Kigoma na kueleza kuwa huo ni muendelezo wa mkakati wa Serikali wa kuufungua ukanda wa magharibi mwa Tanzania kwa njia ya anga.

  • RAIS SAMIA AIFUNGUA BARABARA YA NYAKANAZI- KABINGO YENYE UREFU WA (km 50)

    Wananchi wampongeza kwa kuufungua zaidi mkoa wa Kigoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan Oktoba 16, 2022 akiwa Wilayani Kakonko, Mkoani Kigoma amefungua rasmi barabara ya Nyakanazi- Kabingo( km.50) ikiwa imejengwa kwa takriban shilingi bilioni 43 na ujenzi wake kusimamiwa na TANROADS. Akizungumza katika ufunguzi wa barabara hiyo , Rais Samia alisema Serikali imeamua kuifungua barabara hiyo, pamoja na kuweka mawe ya msingi, ikiwa ni juhudi za Serikali za kuleta maendeleo kwa wananchi. " Tuko katika. ziara Mkoani Kigoma, tumeanza na wilaya ya Kakonko, Mradi wa maji Kakonko,, Hii ni ishara kubwa Serikali imeamua kuleta maendeleo" Alisema Mhe. Rais. Aliongeza " Ufunguzi wa barabara ya Nyakanazi- Kabingo ni moja ya ahadi za Serikali kurahisisha shughuli za kibiashara kwa wananchi. Pia uwepo wa miradi mbalimbali itasaidia kukuza maendeleo kwa wananchi na wananchi waendelee kuchapa kazi kwa bidii". Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Makame Mbarawa alisema ujenzi wa barabara hiyo ni kichocheo kikubwa cha uchumi, na kumpongeza Rais Samia kwa kazi kubwa aliyofanya hadi kukamilika kwa mradi huo. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi wa Kakonko wamepongeza juhudi za Rais Samia na Serikali anayoiongoza kwa kuufungua zaidi mkoa wa Kigoma hususan katika sekta ya ujenzi wa miundombinu ya barabara. Barabara ya Nyakanazi- Kabingo inaunganisha Mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, na Mwanza na pia kuunganisha nchi jirani za Burundi kupitia mpaka wa Manyovu. Ujenzi wa barabara hiyo ni mkakati wa Serikali kuhakikisha barabara zote zinaunganisha mikoa na nchi jirani, pamoja na zile za ndani zinajengwa kwa kiwango cha lami.

  • NAIBU WAZIRI KWANDIKWA AWAPONGEZA TANROADS KUDHIBITI VITENDO VYA RUSHWA.

    Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa (Mb), amewapongeza Wakala wa barabara nchini (TANROADS), kwa mikakati wanayotumia kudhibiti vitendo vya rushwa katika vituo vya mizani hapa nchini.

  • KWANDIKWA: ATEMA CHECHE KWA MKANDARASI KUONGEZA MITAMBO NA WAFANYAKAZI

    Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mheshimiwa Elias Kwandikwa (Mb), ametoa muda wa siku 21 kwa Mkandarasi Nyanza Road Works kuongeza vifaa vya kazi na wafanyakazi ili kuongeza kasi ya ujenzi wa barabara ya Nyakanazi-Kibondo yenye urefu wa KM 50 inayojengwa kwa kiwango cha lami.

  • KWANDIKWA: ACHENI VITENDO VYA HUJUMA MIRADI YA UJENZI

    Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa (Mb), amewataka wananchi wanaopata nafasi za kazi katika miradi ya ujenzi wa barabara kuwa wazalendo katika kulinda vifaa na kuepuka vitendo vya hujuma vinavyoweza kujitokeza ili kuhakikisha miradi hiyo inaenda kwa kasi na kumalizika kwa muda uliopangwa.

    Mhe. Kwandikwa ametoa kauli hiyo wilayani Kasulu mkoani Kigoma, alipokuwa akikagua ujenzi wa barabara ya Kidahwe-Kasulu KM 63 inayojengwa na mkandarasi wa Kampuni ya China Railway 15 Bureau Group Corporation na kuelezwa kuwa kuna wizi wa mafuta kiasi cha lita elfu 23 zilizoibiwa hivi karibun ambapo amewataka wananchi kuwa na uzalendo kwanza katika miradi yote ya ujenzi katika maeneo yote.

    "Wizi wa namna hii haukubaliki na mtandao ni mkubwa hivyo naagiza vyombo vya usalama vichukue hatua kali mapema ili kuweza kuondoa madhara makubwa zaidi", amesema Naibu Waziri Kwandikwa.

    Amewataka makandarasi na wasimamizi wa miradi kutoa elimu kwa waajiriwa kila siku kabla ya kuanza kazi kukemea tabia za wizi na ubadhilifu wowote utakaowezea kutokea kwani ni moja ya sababu za miradi pia kuchelewa na gharama kuongezeka.