-
Welcome
-
PAC YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA BRT III
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) wameishauri Serikali kupitia kuangalia uwezekano wa kufanya maboresha katika eneo la daraja la Mfugale TAZARA kwenye makutano ya barabara ili kuondokana na msongamano mkubwa wa magari pindi mradi wa mabasi yaendayo haraka utakapo kamilika.
-
NAIBU WAZIRI ENG. KASEKENYA ARIDHISHWA NA MAANDALIZI UJENZI WA BRT III
NAIBU Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Eng. Godfrey Kasekenya ametembelea Ujenzi wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka BRT na kueleza kuridhishwa kwake na maandalizi ya kuanza kwa ujenzi wa awamu ya tatu ya mradi huo kutokea Katikati ya Jiji la Dar es Salaam kwenda Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere hadi Gongolamboto KM 24.3.
-
PROF. MBARAWA ARIDHISHWA UJENZI BARABARA DAR ES SALAAM
PROF. MBARAWA ARIDHISHWA UJENZI BARABARA DSM WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ameelezea kuridhishwa kwake na Ujenzi wa Barabara ya Mabasi yaendayo haraka – (BRT) sehemu ya Katikati ya Jiji kwenda Mbagala na kumtaka mkandarasi anaejenga Barabara hiyo kuhakikisha inakamilika kama ilivyo pangwa. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Prof. Mbarawa amesema katika kipindi cha miezi mitatu kutoka sasa anatarajia barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 20.3 itakuwa imefunguliwa yote kwa matumizi. “Nia ya Serikali ni kupunguza msongamano Dar es Salaam hivyo nakuagiza TANROADS na Mkandarasi kuhakikisha sehemu inayokamilika magari yaruhusiwe kuitumia wakati ujenzi unaendelea ili kupunguza msongamano na kuleta ufanisi katika huduma za usafiri na uchukuzi katikati ya jiji la Dar es Salaam,” amesisitiza Prof. Mbarawa. Aidha amewataka madereva wa magari katika barabara ambazo ujenzi wake bado unaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wakandarasi ili kulinda usalama wa abiria, wajenzi na magari kwa ujumla. “…Hatuitaji ajali zitokee hivyo tutii maelekezo ya wataalam wetu yenye nia ya kupunguza msongamano na kulinda usalama wa watu na magari,” amesema Prof. Mbarawa. Prof. Mbarawa amesema ujenzi wa Barabara na Magaraja jijini Dar es Salaam unafanywa kwa awamu hivyo wananchi waendelee kuiunga mkono Serikali ili kufikia malengo tarajiwa yaliokusudiwa. Kwa upande wake, Meneja Mradi wa BRT, Eng. Barakaeli Mmari amesema ujenzi wa Daraja la Juu sehemu ya Chang’ombe makutano ya barabara za Nyerere na Kawawa uko sahihi kulingana na usanifu wake, lengo ni kutoa nafasi katikati kwa magari yaendayo haraka. Amezungumzia umuhimu wa raia wema kupata taarifa sahihi kwa TANROADS pale wanapoona katika miradi hiyo kuna jambo linaloitaji ufafanuzi. Naye Mbunge wa Temeke, Mhe. Doroth Kilave ameishukuru Serikali na kuipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kutokana na kasi ya ujenzi wa miadi hiyo katika jimbo lake. Takribani Shilingi Bilioni 262 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa Barabara ya kupunguza msongamano ya Kilwa na Daraji la Chang’ombe katika makutano ya Barabara za Nyerere na Kawawa jijini Dar es Salaam.
-
WAZIRI MBARAWA ARUHUSU MAGARI KUPITA BARABARA YA JUU CHAN'GOMBE
WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa leo ameruhusu kuanza kutumika kwa njia moja ya barabara ya Juu Chang'ombe ili kupunguza msongamano wa magari katika Barabara ya Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kabla ya kuanza kutumika kwa barabara hiyo, Prof. Mbarawa amemtaka Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS), Eng. Rogatus Mativila kushirikiana na Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani kuhakikisha magari yanayotumia njia hiyo kwa sasa yanazingatia sheria za mwendo kwani bado ujenzi unaendelea eneo hilo.
Alisema kutumika kwa barabara hiyo kutasaidia kupunguza msongamano hivyo, kuwasaidia watumiaji wa barabara hiyo wapate muda wa kutosha kufanya shughuli zao kwani msongamano katika eneo hilo unawapotezea muda.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Eng. Mativila amemhakikishia Mhe. Waziri Mbarawa kuwa ujenzi wa barabara hiyo ambayo ni Awamu ya Pili ya Mradi wa Mabasi yaendayo kwa haraka BRT2 utakamilika kwa ubora na kwa wakati.
Eng. Mativila amesema ujenzi wote wa Barabara za Juu za Chang'ombe na Chuo cha Uhasibu unatarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu. -
GARI KUANZA KUPITA UPANDE MMOJA BARABARA YA JUU UHASIBU, CHANG'OMBE.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa, amesema kuwa wakati ujenzi barabara za juu eneo la Uhasibu na Chang’ombe ukiwa unaendelea gari zitaruhusiwa kupita upande mmoja wa barabara kuanzia Mei 30, mwaka huu.
-
DARAJA LA TANZANITE INAVYOTATUA MSONGAMANO DAR ES SALAAM
RAIS Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Watanzania kuwa Serikali
-
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ARIDHISHWA NA UJENZI WA DARAJA JIPYA LA SELANDER
Rais Samia Suluhu Hassan ameridhishwa na teknologia iliyotumika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi na kupanda kwa kina cha bahari katika kingo za Daraja jipya la Selander lenye urefu wa mita 1030.
-
WAZIRI KAMWELWE ATOA SIKU SABA KWA MHANDISI MSHAURI KUPELEKA KAZI TANROADS
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, atoa siku saba kwa mhandisi mshauri kutoka kampuni ya Studi International aliyefanya usanifu wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Msalato mjini Dodoma, kukabidhi nyaraka za usanifu huo kwa Wakala wa Barabara (TANROADS).
-
PROFESA MBARAWA: MRADI WA UJENZI UBUNGO- KIBAHA KUIPAISHA NCHI KIUCHUMI
SERIKALI imesema mradi wa ujenzi wa barabara ya njia sita kutoka Ubungo hadi Kibaha Mkoani Pwani yenye urefu wa kilometa 16 unaotarajia kuanza mwishoni mwa mwezi Desemba mwaka huu utasaidia kukuza uchumi kwa kuongeza kasi ya usafirishaji wa bidhaa katika nchi jirani kupitia bandari ya Dar es Salaam.
-
BARABARA YA KIMARA BARUTI-CHUO KIKUU KUKAMILIKA NDANI YA SIKU 60
Serikali imetoa siku 60 kwa mkandarasi wa Kampuni ya Hari Singh & Sons kumaliza ujenzi wa kipande cha barabara cha kilomita 1.5 kilichobaki kwa kiwango cha lami katika barabara ya Kimara Baruti-Msewe-Chuo Kikuu yenye jumla ya urefu wa kilomita 2.6.
-
Ujenzi wa Interchange kwenye makutano ya Ubungo
Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), leo umetiliana saini na kampuni ya M/S China Civil Engeneering Construction Cooperation kutoka China (CCECC) mkataba wa ujenzi wa barabara za Juu ‘Interchange’ katika makutano ya barabara ya Sam Najoma na Mandela Ubungo jijini Dar es salaam.