• Welcome

  • WAZIRI BASHUNGWA AKAGUA UREJESHAJI WA MAWASILIANO YA BARABARA MKURANGA, AELEZA MIKAKATI YA SERIKALI

    WAZIRI BASHUNGWA AKAGUA UREJESHAJI WA MAWASILIANO YA BARABARA MKURANGA, AELEZA MIKAKATI YA SERIKALI

  • UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA KUFUNGUA FURSA MAFIA

    UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA KUFUNGUA FURSA MAFIA

  • WAZIRI BASHUNGWA AAGIZA WAHANDISI WASHAURI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA MAKANDARASI KUTOPEWA KAZI

    WAZIRI BASHUNGWA AAGIZA WAHANDISI WASHAURI WANAOSHINDWA KUSIMAMIA MAKANDARASI KUTOPEWA KAZI

  • Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia kutekeleza miradi tisa ya kimkakati mkoani Pwani

    Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia kutekeleza miradi tisa ya kimkakati mkoani Pwani

  • BASHUNGWA: RAIS DKT. SAMIA YUPO 'SERIOUS' NA UJENZI WA BARABARA NCHINI

    Waziri wa Ujenzi Mhe. Innocent Bashungwa amesema ujenzi wa miundombinu ya barabara nchini unafanyika kwa umakini na viwango vya ubora chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
    Waziri Bashungwa ameyasema hayo leo Septemba 20, 2023 mbele ya wananchi wa Ikwiriri mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa mikoa ya Kusini.
    "Sisi kazi yetu ni kutekeleza yale ambayo Mhe. Rais ametuagiza, kwenye maelekezo uliyotupatia ya utiaji saini mikataba mbalimbali ambayo inakaribia trilioni 2 hata TARURA watakuwepo kuonesha namna Serikali yako ilivyojipanga katika ujenzi wa barabara", amesema Mhe. Bashungwa.
    Katika hatua nyingine Waziri Bashungwa amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza upembuzi yakinifu wa ujenzi wa Barabara ya Mabasi yaendayo haraka kutoka Mbagala - Vikindu ufanyike haraka ili utaratibu wa kuanza ujenzi uanze mara moja.
    "Mhe. Rais BRT kutoka Mbagala rangi tatu hadi vikindu umetuelekeza usanifu ufanyike haraka ili barabara hiyo na njia nne ije mpaka Vikindu ili wananchi wa mkoa wa hapa Pwani na Rufiji waweze kuingia Dar es Salaam kwa wepesi na kutoka kwa wepesi"- amesema Mhe. Bashungwa.
    Naye Mbunge wa Rufiji ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Mohammed Mchengerwa amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia kutoa kiasi cha Shilingi Bilioni 75 kuanza ujenzi wa barabara ya Nyamwage - Utete yenye urefu wa kilometa 37 na tayari wakandarasi wanaendelea na ujenzi wa barabara hiyo.
    "Naomba nichukue nafasi hii kukushukuru Mhe. Rais kwa kuridhia kujenga barabara ya Ikwiriri- Mkongo kwa kiwango cha lami na tayari mkandarasi yupo site amekwishaanza kujenga daraja la mbambe na barabara itakayotoka mbambe kuja hapa Ikwiriri mjini"- ameongeza Mhe. Mchengerwa.

  • DARAJA JIPYA LA WAMI LAANZA KUTUMIKA

    Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ameruhusu Magari kuanza kutumia daraja jipya la Wami kufuatia ujenzi wake kukamilika kwa asilimia 96. Waziri Mbarawa amewetaka madereva na watumiaji wa daraja walitunze ili liweze kudumu miaka 120 kama lilivyo sanifiwa. “Sisi kama Wizara, TANROADS pamoja na wananchi wa maeneo haya tuna kazi kubwa ya kulinda Daraja hili, ili tuwatende haki Watanzania wenzetu na vizazi vya baadae”. Alisema Prof Mbarawa. Aidha Prof. Mbarawa aliongeza kwa kusema “Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi inasimamia miradi mbalimbali ya kimkakati nchi nzima kwa lengo la kuifungua nchi kiuchumi na kwa miradi ya Pwani ifikapo mwaka 2025 barabara ya Bagamoyo – Pangani – Tanga – Horohoro hadi Lungalunga (Kenya) itakuwa imekamilika”. ” Serikali pia itajenga barabara za kisasa ya magari yaendayo haraka kuanzia Kibaha – Chalinze – Morogoro Express Way yenye urefu wa kilometa 215” alisema Prof. Mbarawa. Kwa upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Eng. Dorothy Mtenga, amesema zaidi ya shillngi billioni 75 zimetumika katika ujenzi wa Daraja Jipya la Wami. Aidha daraja la zamani lilikuwa halikidhi mahitaji ya magari yanayopita kwa kuwa lilijengwa miaka 63 iliyopita na lilikuwa na njia moja. Naye Mkuu wa Wilaya wa Bagamoyo, Bi Zainabu Abdallah Issa, ameishukuru Serikali hususan Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa utekelezaji wa miradi ya miundombinu. Amemhakikisha Waziri Mbarawa kuwa madaraja na barabara zinazojengwa katika mkoa wa Pwani zinatunzwa vizuri. Kwa upande wake Mbunge wa Chalinze ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Ridhiwani Kikwete, ameishukuru Serikali kwa kuendeleza miradi ya miundombinu katika mkoa wa Pwani ili kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo. Daraja jipya la Wami, lenye urefu wa mita 513.5, upana mita 11.85 na barabara unganishi km 3.8 linaunganisha mkoa wa Pwani na Tanga. Kukamilika kwake kutachochea fursa zaidi za kiuchumi na kuleta maendeleo kwa mikoa ya kaskazini mwa Tanzania