MADARAJA YALIYOKAMILIKA NA YANAYOENDELEA: MAENDELEO MAKUBWA YA MIUNDOMBINU YA TANROADS
30 Machi, 2026
Hayo yameelezwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa TANROADS, Mhandisi Ephatar Mlavi, Tarehe 30 Machi, 2026 katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) katika jingo la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo, Dodoma. Ambapo ameeleza mafanikio makubwa katika ujenzi wa madaraja Nchini.
TANROADS imekamilisha madaraja muhimu Ikiwa ni pamoja na Daraja la J.P. Magufuli, Daraja la Tanzanite, Daraja la Msingi, Daraja la Wami, Daraja la Kiyegeya, Daraja la Kitengule, Daraja la Gerezani, na Daraja la Ruhuhu. Madaraja haya yameimarisha usafiri na kuunganisha maeneo, kuchochea biashara na maendeleo ya kijamii.
Zaidi, TANROADS inaendelea na ujenzi wa madaraja mengine 17 katika mikoa mbalimbali. Madaraja haya ni pamoja na Daraja la Pangani, Daraja la Mirumba, Daraja la Mbangala, Daraja la Simiyu, Daraja la Mbambe, Daraja la Doma, Daraja la Nzali, Daraja la Chakwale, Daraja la Nguyami, Daraja la Suguta, Daraja la Sukuma, Daraja la Jangwani, Daraja la Mwanjiri, Daraja la Mkili, Daraja la Kalebe, Daraja la Kavuu, na Daraja la Mitomoni. Haya madaraja yanaendelea katika hatua mbalimbali za ujenzi.